explain-icon

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa muislamu atakapovaa khofu zake baada ya kutawadha, kisha akatengukwa udhu baada ya hapo, na akataka kutawadha, basi anatakiwa afute juu yake akitaka kufanya hivyo, na aswali nazo wala asizivue kwa muda maalum, isipokuwa atakapopatwa na janaba hapo atalazimika kuvua khofu na kuoga.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Hairuhusiwi kufuta juu ya khofu mbili isipokuwa baada yakuwa na twahara kamili.
  • Muda wa kufuta kwa mkazi: Ni mchana na usiku (Masaa 24), na kwa msafiri: Ni michana mitatu na usiku wake (Masaa 72).
  • Kufuta juu ya Khofu mbili kunahusu tu hadathi ndogo nasi kubwa, ama hadathi kubwa haitakiwi kufuta, bali ni lazima kuvua khofu mbili na kuosha miguu miwili.
  • Ni sunna kuswali na viatu na khofu na mfano wake na hii ni kwa sababu ya kwenda kinyume na Mayahudi, na hii ni pale viatu vitakapokuwa twahara (visafi), na havina udhia kwa wenye kuswali, au msikiti, mfano kama miskiti iliyotandikwa mabusati mtu hatakiwi kuswali navyo.
  • Kufuta juu ya khofu mbili kuna urahisi na wepesi kwa umma huu.