Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-amekaa kati ya Maswahaba zake, akasema: Huu ndiyo wakati ambao itaondolewa na kupokonywa elimu kutoka kwa watu, Hivyo akashangaa Ziyaad Bin Labiid Al-Answaariy-Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na akamuuliza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, Akasema: Ni vipi itaondolewa elimu na kutupotea sisi?! Na hali yakuwa tumeisoma Qur'ani na tukaihifadhi; Namuapia Mwenyezi Mungu kuwa tutaisoma, na kuwasomesha wake zetu na watoto wetu, na wajukuu wetu, Akasema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akiwa anaona ajabu: Amekukosa mama yako ewe Ziyaad! kama ikiwa nitakuzingatia wewe ni katika wajuzi wa mji wa Madina! Kisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-akaweka wazi kuwa kuiokosa elimu siyo kuikosa Qur'ani, bali kukosa elimu ni kuacha kuifanyia kazi, Kwa mfano hii hapa Taurati na Injili ipo kwa Mayahudi na Manaswara; na pamoja na hivyo haiwanufaishi, wala hawapati faida kutokana na makusudio yake; na faida yenyewe ni kufanyia kazi walicho jifunza.