Ameeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa miongoni mwa alama za Kiyama ni kukaribiana zama. Mwaka utapita kama mwezi unavyopita, Na mwezi utapita kama inavyopita wiki, Na wiki itapita kama inavyopita siku. Na siku itapita kama inavyopita saa moja, Na saa itapita upesi kama linavyochomwa jani kavu la mtende.