Taabii (Mwanafunzi wa Maswahaba) Malik bin Ausi anaeleza kuwa alikuwa na dinari za dhahabu, na alitaka kuzibadilisha kwa dirham za fedha, basi Twalha bin Ubaidillah (radhi za Allah ziwe juu yake) akamwambia: Tupe dinari zako nizione! Kisha akamwambia baada ya kuamua kununua: Njoo kwetu ikiwa mtumwa wetu atakuja baadaye tutakupe dirham za fedha, Omari bin Khattab Mwenyezi Mungu amuwie radhi, alilaani aina hii ya muamala (biashara), na akaapa kwa Twalha kuwa atalipa fedha sasa, au amrudishie dhahabu yake aliyoichukua yeye, akasema kuwa kuuza fedha kwa dhahabu, au kinyume chake, lazima kupokea kuwe mkono kwa mkono, vinginevyo biashara hiyo itakuwa ni riba iliyoharamishwa na uuzaji batili, Dhahabu haiuzwi kwa fedha, wala fedha kwa dhahabu, isipokuwa mkono kwa mkono, na kufanyike kubadilishana, wala haiuzwi kwa ngano, na shayiri kwa shayiri, na tende kwa mfano wake, kipimo kwa kipimo, mkono kwa mkono; na haijuzu kuachana katika makubaliano kabla ya kuimiliki.