Mtu mmoja kipofu alimjia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hakika mimi sina wa kunisaidia na kunishika mkono kuja msikitini, katika swala tano, akitaka Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amruhusu, alipompa mgongo alimuita na akasema: Je, unasikia adhana ya swala? akasema: Ndiyo, akasema: Basi mjibu anayenadi kwa ajili ya swala.