Alieleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa safu bora kwa wanaume katika swala na yenye malipo makubwa na fadhila kubwa ni ya kwanza; kwakuwa watu wanakuwa karibu na imam na pia kusikiliza kisomo chake nakuwa kwao mbali na wanawake, na ya shari na yenye malipo na fadhila ndogo na iliyombali na matakwa ya sheria ni ya mwisho, na safu bora kwa wanawake ni safu ya mwisho; kwa sababu ndio inayowasitiri vizuri kwao, na iko mbali na kuchanganyikana na wanaume na macho yao na kufitinika nao, na safu ya shari ni ya kwanza; kwakuwa inakuwa karibu na wanaume na ni kujitia katika fitina.