Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alichukua ahadi na mkataba kutoka kwa Masahaba ya utii kwa wenye mamlaka na watawala katika wepesi na ugumu, na katika hali ya utajiri na umasikini, na sawa sawa amri zao ziwe katika yale wanayoyapenda au kuyachukia, hata kama watawala watajipendelea kuliko raia kwa mali ya umma au vyeo au mengineyo, basi ni wajibu kwao kusikiliza na kutii katika wema, na wasitoke dhidi yao, kwa sababu fitina na ufisadi katika kupigana nao ni mambo makubwa na ni mabaya mno kuliko ufisadi unaotokea kwa sababu ya dhulma zao, na katika mambo waliyoyachukulia kiapo ni waseme kweli mahali popote, wakilitakasa hilo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hawamuogopi mwenye kuwalaumu.