Aliambiwa Osama bin Zaid Mwenyezi Mungu awawie radhi wote wawili: Hivi huendi kwa Othman bin Affan, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, ukamwambia kuhusu fitina zilizotokea baina ya watu na kutafuta kuzizima. Basi akawaeleza kuwa alizungumza naye kwa siri ili kutafuta maslahi, si kuchochea kwa fitina, na lengo lake lilikuwa kwamba hataki kuwashutumu viongozi hadharani, ikawa ni sababu ya kurefusha mzozo kwa kiongozi, na ni mlango wa fitina na uovu, na siwezi kuwa wa kwanza kuufungua. Kisha Osama Mwenyezi Mungu awawie radhi, akasema kuwa: Anawanasihi viongozi kwa siri na wala hambembelezi yeyote kwa kumsifu, hata akiwa kiongozi, na wala hawabembelezi kwa kuwasifu kwa uongo, na hiyo ni baada ya yeye kuwa alisikia kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa ataletwa mtu Siku ya Kiyama na kutupwa Motoni, na utumbo wake utatoka nje ya tumbo lake kutokana na ukali wa adhabu, na atasokota utumbo wake katika hali hii Motoni kama punda anayezunguka jiwe lake la kusagia nafaka, watu wa Motoni watamzunguka kwa duara kisha watamuuliza: Ewe fulani, je si wewe aliyekuwa ukiamrisha mema na kukataza maovu?! Atasema: Mimi nilikuwa nikiamrisha mema na wala siyafanyi, na ninakataza maovu na ninayafanya.