explain-icon

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa Moto umezungukwa na kuzingirwa na mambo ambayo nafsi inayatamani, kama kufanya maharamisho au uzembe katika mambo ya wajibu; Atakayeendekeza matamanio ya nafsi yake katika hilo atastahiki moto, nakuwa Pepo imezungukwa na kuzingirwa na mambo ambayo yanachukiwa na nafsi; kama kudumu katika maamrisho na kuacha maharamisho na kuvumilia juu ya hilo, atakapovumilia na akapigana vita na nafsi yake juu ya hilo atastahiki kuingia Peponi.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Miongoni mwa sababu za kuingia katika matamanio ni shetani kuyapamba maovu na machafu, mpaka nafsi inayaona kuwa ni mazuri na kisha kuyaelekea.
  • Amri ya kujitenga mbali na matamanio yaliyoharamishwa; kwa sababu hayo ni njia ya kuelekea motoni, na kuvumilia juu ya kero; kwani ni njia ya kuelekea Peponi.
  • Ubora na fadhila za kupigana na nafsi na kuwa na bidii katika ibada na kuvumilia kero na tabu zinazo zizunguka ibada.