Amekataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuweka nadhiri, nayo ni mtu kujiwajibishia kitu ambacho sheria haijamlazimisha kukifanya, na akasema kuwa: Nadhiri haiwahishi kitu na wala haikicheleweshi, bali hutolewa vilivyo kwa mtu bahili ambaye hafanyi ila yale ya wajibu pekee, nakuwa nadhiri haileti kitu ambacho hakikukadiriwa.