Mtume, rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akinyanyua mikono yake katika sehemu tatu wakati wa kuswali, usawa wa mabega ni: Pale panapounga kati ya mfupa wa bega na mkono. Sehemu ya kwanza: Anapofungua swala wakati wa takbira ya kuhirimia swala. Sehemu ya pili: Anapotoa takbira kwa ajili ya rukuu. Sehemu ya tatu: Anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu, na akasema: Sami'allahu liman hamidah, Rabbanaa walakal hamdu. Amemsikia Mwenyezi Mungu mwenye kumhimidi, Mola wetu Mlezi, na sifa njema ni zako. Na alikuwa hanyanyui mikono yake wakati wa kuanza kusujudu, wala wakati wa kunyanyua kutoka katika sijida.