Kutoka kwa Hudhaifa -Radhi za Allah ziwe juu yake-: Yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema kati ya sijida mbiliL "Rabbigh-firlii, Rabbigh-firlii".
Sahihi - Imepokelewa na Abu Daud, Nasai, Ibn Majah na Ahmad
Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema wakati wa kikao kilichopo baina ya sijida mbili: Rabbigh-firlii, Rabbigh-firlii.
Na maana ya Rabbigh-firlii: Ni mja kuomba kutoka kwa Mola wake ayafute madhambi yake na asitiri aibu zake.
Katika Faida za Hadithi
Sheria ya dua hii kati ya sijida mbili katika swala ya faradhi na sunna.
Inapendeza kuirudiarudia kauli ya Rabbigh-firlii, ila wajibu ni kuisema mara moja.