explain-icon

Ufafanuzi

Alimuona Mtume Rehema na amani ziwe juu yake mtu mmoja akila kwa mkono wake wa kushoto, akamuamrisha ale kwa mkono wake wa kulia, Yule bwana akamjibu kwa kiburi na kwa kuongopa kuwa hawezi! Mtume Rehema na amani ziwe juu yake akamuombea dua mbaya azuiliwe kula kwa mkono wa kulia, Mwenyezi Mungu akajibu dua ya Nabii wake, kwa kupooza mkono wake wa kulia, hakuweza kuunyanyua kwenda kinywani kwake baada ya hapo kwa chakula au kinywaji.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Uwajibu wa kula kwa mkono wa kulia, na uharamu wa kula kwa mkono wa kushoto.
  • Kiburi katika kutekeleza hukumu za sheria mwenye kufanya hivyo anastahiki adhabu.
  • Ukarimu wa Mwenyezi Mungu kwa Nabii wake Muhammadi Rehema na amani ziwe juu yake kwa kujibu maombi yake.
  • Sheria ya kuamrisha mema na kukataza maovu kwa kila hali hata wakati wa chakula.