Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa shukurani za mja kwa Mola wake Mlezi juu ya fadhila zake na neema zake ni miongoni mwa mambo ambayo huleta radhi za Allah; akala chakula akasema: Al-hamdulillah, na akanywa kinywaji na akasema: Al-hamdulillah.