explain-icon

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa kumtaja Allah Mtukufu kwa maneno haya matukufu ni bora kuliko dunia na vilivyomo, na utajo huo ni kusema: "Sub-haana llaah": Ni kumtakasa Mwenyezi Mungu kutokana na mapungufu. "Alhamdulillaah": Ni kumsifia kwa sifa za ukamilifu pamoja na kumpenda na kumtukuza. "Laa ilaaha illa llaah": Hakuna muabudiwa wa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu. "Allaahu Akbaru: Mkubwa na Mtukufu kuliko kila kitu.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Himizo la kumtaja Mwenyezi Mungu, nakuwa hilo linapendeka zaidi kuliko vyote vilivyochomozewa na jua.
  • Himizo la kukithirisha dhikiri; kwakuwa ndani yake kuna malipo na fadhila kubwa.
  • Starehe za dunia ni ndogo na matamanio yake ni yenye kuondoka.