explain-icon

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa yanayomsibu muislamu katika maradhi na msongo na huzuni na misukosuko na majanga na shida mbali mbali na hofu na njaa, hata kama utakuwa ni mwiba utakaomchoma na kumuumiza, hilo kwake linakuwa ni kafara ya madhambi kwake na kifuta makosa.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Kumebainishwa fadhila ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake waumini na huruma yake kwao kwa kuwasamehe madhambi hata kwa madhara madogo yanayowasibu.
  • Ni lazima kwa muislamu ataraji malipo kwa Allah kwa yale yanayomsibu, na asubiri kwa dogo na kubwa, ili iwe ni sababu ya kunyanyuliwa daraja na ni kafara ya makosa.