Anaeleza swahaba Jariiri Bin Abdallah radhi za Allah ziwe juu yake yakuwa yeye alishikamana na maamrisho na akampa ahadi Mtume rehema na amani ziwe juu yake juu ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kutekeleza swala tano za faradhi usiku na mchana, kwa kutimiza sharti zake na nguzo zake na wajibu zake na sunna zake, na kutelekeza zaka ya wajibu, nayo ni ibada ya mali ya lazima, huchukuliwa toka kwa matajiri na kupewa wanaostahiki katika mafakiri na wengineo, na kuwatii viongozi, na kumpa nasaha kila muislamu, na hii ni kwa kuchunga masilahi yake, na kumfikishia kheri, na kumkinga na shari kwa kauli na vitendo.