Walimuuliza maswahaba Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- : Ni swala ipi bora? Na swali hili ni kwasababu ya pupa yao ya kuhakikisha wanapata kiwango kikubwa cha mema,Na makusudio yake:Ni aina ipi ya swala zote ndio bora? Au: Yaani ni tendo lipi katika matendo ya swala ndio bora? Ni kusimama au kurukuu au kusujudu? Akaeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa ni kurefusha kisimamo ndani yake.