Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa atakapotoa mtu matumizi kwa familia yake, wale anaolazimika kuwahudumia kama mke wake na watoto wake na wengineo huku akijikurubisha kwa Allah Mtukufu kwa hilo, na akitaraji malipo kwake kwa yale anayowahudumia basi atakuwa na malipo ya sadaka.