explain-icon

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- katika baadhi ya safari zake, na watu wakiwa mahali pao pa kulala wanapopumzikia katika vipandwa vyao na mahema yao, akamtuma mtu kwenda kwa watu akawaamrishe wakate vikamba vinavyotundikwa kwa wanyama sawa sawa ziwe zimetokana na kamba ya upinde -kamba ya upinde, au kinginecho kama kengele au kiatu, na hii ni kwa sababu walikuwa wakitundika kwa kuogopa kijicho, wakaamrishwa kuvikata; kwa sababu havizuii kwao chochote, nakuwa manufaa na madhara yako mkononi mwa Allah peke yake asiye na mshirika.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Uharamu wa kutundika makamba na kengele kwa ajili ya kuleta manufaa au kuzuia madhara; kwani hilo ni katika ushirikina.
  • Kufunga kengele isiyoambatana na itikadi, kwa ajili ya urembo, au kuongozea mnyama au kumfungia haina tatizo.
  • Uwajibu wa kukemea uovu kulingana na uwezo.
  • Uwajibu wa moyo kuambatana na Allah peke yake asiye na mshirika.