Kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Tulikuwa pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake ghafla akasikia kishindo, akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: “Je, mnajua ni nini hiki?” Akasema: Tukasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanajua zaidi, akasema: «Hili ni jiwe lililotupwa Motoni muda wa (miaka) sabini iliyopita, na sasa linaanguka Motoni mpaka litafika katika kina chake. Sahihi - Imepokelewa Imamu Muslim
explain-icon

Ufafanuzi

Mtume rehema na amani ziwe juu yake alisikia sauti ya kushtua kama kuanguka kwa mwili, akawauliza Masahaba aliokuwa nao Mwenyezi Mungu awawie radhi kuhusu sauti hiyo, wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi zaidi. Akawaambia rehema na amani ziwe juu yake: Sauti hii mliyoisikia ni ya jiwe lililorushwa kutoka ukingo wa Jahannam miaka sabini iliyopita lilikuwa likiporomoka na kuanguka humo, hivi sasa mliposikia kishindo ndio limefika katika kina chake.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Himizo la kujiandaa na siku ya mwisho kwa amali njema, na kutahadhari na Jahannam.
  • Ni sunna kuiegemeza elimu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika yale ambayo mtu hana elimu nayo.
  • Mwalimu anatakiwa kuamsha hisia na umakini kwa wanafunzi kabla ya kuwaeleza; ili uwe ni msukumo wa wao kuelewa.