explain-icon

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa wanaohukumu kwa uadilifu na haki baina ya watu walio chini ya utawala wao na hukumu zao, na familia zao, nikuwa watakaa katika makao ya juu zaidi yaliyoumbwa kwa nuru, ikiwa ni takrima kwao siku ya Kiyama. Na mimbari hizi ziko kuliani mwa Allah Mtukufu, na mikono yake miwili Mtukufu yote ni kulia.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Fadhila za uadilifu na himizo juu yake.
  • Uadilifu ni neno la kiujumla linalokusanya tawala zote, na hukumu za kati ya watu hata uadilifu kati ya wake na watoto, na mengineyo.
  • Kumebainishwa nafasi ya waadilifu siku ya Kiyama.
  • Kutofautiana kwa makazi ya watu wa imani siku Kiyama kila mmoja atakuwa kulingana na matendo yake.
  • Mfumo wa kuhamasisha ni katika njia za kufanya da'wa zinazomvutia mwenye kulinganiwa kuja katika utiifu.