explain-icon

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka huteremka kila usiku katika mbingu ya dunia pindi inapobakia theluthi ya mwisho ya usiku, na anawahamasisha waja wake wamuombe, kwani yeye anamjibu mwenye kumuomba, na anawahimiza wamtake haja zao, kwani yeye humpa anayemuomba, na anawaita wamuombe msamaha kutokana na madhambi yao kwani yeye huwasamehe waja wake waumini.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Ubora wa theluthi ya mwisho ya usiku na swala na dua na kutaka msamaha ndani yake.
  • Ni wajibu kwa mwanadamu wakati wa kusikia hadithi hii awe na pupa kubwa ya kunufaika na nyakati za kujibiwa dua.