Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema katika Hadithil Kudsi: Ananiudhi na ananishusha hadhi mwanadamu anayetukana na kusema vibaya wakati wa kufikwa na matatizo na machukizo; kwa sababu yeye Mtukufu ndiye mpangiliaji peke yake na muendeshaji wa yote yanayotokea; kutukana nyakati ni kumtukana Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, na nyakati ni kiumbe na kinaendeshwa, yanatokea matukio ndani yake kwa amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.