Ametahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuapa na kukithirisha kiapo hata kama mtu akiwa mkweli katika kuuza na kununua, na akaeleza kuwa ni sababu ya kuondoka bidhaa na mzigo, lakini hilo hupunguza na kubatilisha baraka za faida na chumo, na anaweza kumpelekea Mwenyezi Mungu namna zitakazoharibu mali yake, ima kuibiwa au kuungua kuangamia au kuporwa au kuvamiwa au majanga mengine yatayoharibu mali yake.