Kutoka kwa bin Omari -radhi za Allah ziwe juu yake yeye na baba yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-: "Mtu yeyote atakayesema kumwambia ndugu yake: Ewe kafiri, basi utampata mmoja katika ya hao wawili, ikiwa atakuwa kama alivyosema (litathibiti hilo), na kama si hivyo utarejea kwake". Sahihi - Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake
explain-icon

Ufafanuzi

Amemtahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake muislamu kusema kumwambia ndugu yake muislamu: Ewe kafiri, basi atakuwa kastahiki neno kafiri mmoja wao, na ikiwa ni kweli kama alivyosema (utamthibitikia), na kama si kweli ukafiri utarejea kwa msemaji aliyesema kumwambia ndugu yake.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Amekemewa muislamu kusema kumwambia ndugu yake muislamu mambo asiyokuwa nayo, kama sifa ya uovu na ukafiri.
  • Tahadhari ya kusema maneno haya machafu, na kwamba msemaji wake yuko katika hatari kubwa atakaposema kumwambia ndugu yake, na lazima kuhifadhi ulimi, na muislamu asizungumze ila kwa elimu.