Alitahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu dhulma, ikiwemo: Kuwadhulumu watu na kujidhulumu mwenyewe na kufanya dhulma katika haki ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, nayo kuacha kumpa kila mwenye haki haki yake, nakuwa dhulma ni giza kwa wafanyaji dhulma siku ya Kiyama ikiwemo kupata matatizo na misukosuko, Na akakataza tamaa ambayo ni ubahili uliopitiliza pamoja na pupa, na ikiwemo kufanya uzembe katika kutekeleza haki ya mali na tamaa iliyopitiliza ya kuipupia dunia, Na aina hii ya dhulma iliwaangamiza Umma waliokuwa kabla yetu, kiasi ambacho iliwapelekea kuuana wao kwa wao, na kuyahalalisha yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu katika mambo yaliyoharamishwa.