Ametahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa yeyote atakayekusudia kujiua katika dunia, basi ataadhibiwa siku ya Kiyama ndani ya Moto wa Jahannamu kwa njia hiyo hiyo aliyoifanya yeye mwenyewe katika dunia, hayo yakiwa ni malipo kulingana na alichokifanya, atakayejirusha mwenyewe kutoka juu ya mlima akajiua, basi atakuwa ndani ya Moto wa Jahannam akidondoka humo katika milima ya Jahannamu na katika mabonde yake milele na mile humo, na atakayejipiga mwenyewe kwa chuma tumboni mwake akajiua, basi chuma chake kitakuwa mkononi kwake akichoma kwa chuma hicho tumbo lake ndani ya Moto wa Jahannam milele na milele humo.