Alilalamika mmoja kati ya Masahaba wa kike kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kuendelea kushuka kwa damu yake, Akamuamrisha aache kuswali kwa kiwango cha siku alizokuwa akikaa hedhi yake kabla ya kushuka jambo hili lililojitokeza kwa dharura, kisha aoge na aswali, akawa akioga kwa hiyari kwa kila swala.