Anaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa: “Balaa na mtihani havikomi kwa muumini wa kiume na wa kike, katika afya yake na mwili wake, na kwa watoto wake, kama magonjwa, kifo, uasi na mengineyo, na katika mali yake kutiwa umasikini, kutoweka kwa biashara, kuibiwa, kuvurugika kwa maisha na dhiki katika riziki, na ugumu wa maisha, mpaka Mwenyezi Mungu atamfutia dhambi zake zote kwa mateso haya, ili atakapokutana na Mwenyezi Mungu atakuwa kasafishika na madhambi na maovu yote aliyoyafanya.