Jariri bin Abdullah Mwenyezi Mungu amuwie radhi, alimuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu mwanaume kumwangalia mwanamke wa kando ghafla bila kukusudia? Basi akamuamrisha rehema na amani ziwe juu yake kuwa aelekeze uso wake pembeni upande wa pili mara anapojua hilo, na hatokuwa na dhambi juu yake.