Anatueleza Mtume rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi kuwa muumini linaweza kutokea kwake jambo lolote katika matatizo, katika nafsi yake au mali yake au kinginecho, nakuwa Mwenyezi Mungu atamlipa juu ya matatizo hayo ikiwa kama yeye atavumilia, nakuwa kila majanga yanavyozidi kuwa makubwa na hatari yake kuwa kubwa ndivyo malipo yake yanavyokuwa makubwa kwa Mwenyezi Mungu, kisha anabainisha rehema na Amani zimfikie kuwa mitihani ni katika alama za kuwapenda Mwenyezi Mungu waumini, nakuwa hukumu ya Mwenyezi Mungu na makadirio yake ni lazima yafanyike hakuna namna, lakini atakayesubiri na akaridhia, basi Mwenyezi Mungu atamlipa kwa hilo kwa kumridhia na zinamtosha zaidi thawabu zake, nakuwa atakayechukia na akakerwa na hukumu ya Mwenyezi Mungu na makadirio yake, basi Mwenyezi Mungu atamchukia na zinamtosha zaidi adhabu zake.