Ameeleza Abdallah bin Masudi radhi za Allah ziwe juu yake ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alilala juu ya busati dogo lililoshonwa kutokana na baadhi ya mimea, akasimama ukiwa tayari mkeka umeathiri katika ngozi ya ubavu wake, tukasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, lau tungelikuandalia godoro laini basi ingelikuwa bora kuliko kujilaza kwako juu ya mkeka mgumu, akasema rehema na amani ziwe juu yake: Sina mapenzi wala hamu ya dunia mpaka niwe na tamaa nayo, kwani mfano wangu mimi na kubakia katika dunia ni kama msafiri aliyejikinga kivulini kwa muda mfupi kisha akaondoka akakiacha.