Amesema Ka'bu bin Iyadh -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Nilimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Akisema: (Hakika kila umma una mtihani wake) Nayo ni ile wanayotahiniwa kwayo na kujaribiwa katika mambo. (Na mtihani wa Umma wangu ni mali) kwasababu ndio unaozuia ukamilifu wa kuandaa marejeo; Hivyo upuuzi hushughulisha hisia na kusimamia mambo ya utiifu na kusahau Akhera.