Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mzee huzeeka na mwili wake kudhoofika, lakini moyo wake huwa kijana kwa kupenda mambo mawili: La kwanza: Kuipenda dunia kwa kuwa na wingi wa mali. La pili: Kuwa na uhai na maisha na umri na matarajio ya muda mrefu.