Mtume rehema na amani ziwe juu yake amemhimiza muislamu kuwa asife isipokuwa katika hali ya kumdhania vizuri Mwenyezi Mungu kwa kuwa na matarajio makubwa ya kheri wakati wa kufikwa na mauti kuwa Mwenyezi Mungu atamhurumia na kumsamehe, kwa sababu hofu hutakiwa kwa ajili ya kufanya vizuri katika matendo, na katika hali hiyo si hali ya kufanya amali yoyote, kinachotakiwa hapo nikuwa na matumaini makubwa.