Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu wema na uovu, akasema: Hakika jambo kubwa zaidi katika wema ni tabia njema pamoja na Mwenyezi Mungu kwa kumuogopa, na pamoja na viumbe kwa kustahamili maudhi yao, na kupunguza hasira, na kukunjua uso, na kuwa na maneno mazuri, na kuunga udugu na utiifu na upole na kuwapa watu udhuru na kuishi nao vizuri na ujamaa mzuri. Nakuwa wema ni ule uliotulizana kwao moyo na nafsi. Na ama dhambi ni katika lile ambalo nafsi itataharuki kutokana na mambo yenye utata na ikapata shaka pasina kukunjuka kifua, na moyo ukapatwa na shaka, na ukaogopa kwakuwa ni dhambi, ukawa haukutaka kulidhihirisha kwakuwa ni jambo baya kwa mtu na kwa watu wengine pia, na hii ni kwa sababu tabia ya nafsi hupenda kutazamwa na watu wengine ikifanya kheri; na hata kama watu watakupa majibu mazuri usichukue majibu yao madamu alama za utata zinazunguka ndani ya nafsi yako majibu yao hayawezi kuondoa utata madamu utata ni wa kweli na akawa anayekupa majibu anatoa pasina elimu; ama ikiwa majibu yanatokana na dalili ya kisheria kilichowajibu kwa mpewa majibu arejee katika hilo, hata kama moyo wake hautokunjuka kwa hilo.