Alikuwa rehema na amani ziwe juu yake anapopiga chafya: Jambo la kwanza: Anaweka mkono wake, au nguo yake juu ya kinywa chake; Kisije kutoka kinywani mwake au puani mwake chochote kitakachomuudhi aliyekaa naye. Jambo la pili: Anashusha sauti yake na wala hainyanyui.