Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa tabia njema humfikisha mwenye tabia hiyo nafasi ya mwenye kufunga mchana daima na kusimama usiku, na tabia njema inakusanywa na: Kutenda wema, na kauli nzuri, na uso mkunjufu, na kuacha maudhi na kuyavumilia kutoka kwa watu.