Aliwaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake Maswahaba kuhusu ushindi wa waislamu kesho dhidi ya Mayahudi wa mji wa Khaibar ambao ni mji uko karibu na Madina, na hii ni kupitia mkono wa mtu atakayempa bendera, nayo ni bendera inayofanywa na jeshi kama nembo, na mtu huyu miongoni mwa sifa zake nikuwa anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanampenda pia. Na alieleza Omari bin Khattwab radhi za Allah ziwe juu yake kuwa hapendi uongozi na hapendi kuwa yeye ndiye anayelengwa isipokuwa kwa siku hiyo; kwa kutaraji yampate aliyoyasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika mapenzi ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Omari akanyanyua mwili wake ili auone Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa kutaraji kuwa anaweza kuitwa kwa ajili ya hilo, na akiwa na pupa na tamaa ya kuchukua bendera hiyo. Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamuita Ally bin Abii Twalib radhi za Allah ziwe juu yake akampa bendera, na Mtume rehema na amani ziwe juu yake akaamrisha jeshi litembee, na lisiondoke katika vita baada ya kukutana na maadui sawa iwe ni kwa mapumziko au kwa kusitisha au kutuliza vita, mpaka Mwenyezi Mungu amfungulie ngome hizi kwa ufunguzi na ushindi. Akatembea Ally radhi za Allah ziwe juu yake, kisha akasimama isipokuwa hakugeuka; ili asiende kinyume na amri ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake, basi Ally radhi za Allah ziwe juu yake akanyanyua sauti yake: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nipigane na watu kwa lipi?. Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: Pigana nao mpaka washuhudie kuwa hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ikiwa watalikubali hilo, na wakaingia ndani ya Uislamu; watakuwa wamezizuia kwako damu zao na mali zao, na zitakuwa haramu kwako, isipokuwa kwa haki yake, yaani: Isipokuwa kama watafanya uhalifu au kosa la jinai watakalostahiki kuuawa kwa kosa hilo kwa mujibu wa hukumu za Uislamu, na hesabu yao itakuwa kwa Mwenyezi Mungu.