Mtume rehema na amani ziwe juu yake anatueleza kuwa siku bora kabisa iliyochomozewa na jua ni Ijumaa, Miongoni mwa sifa zake: Mwenyezi Mungu alimuumba Adam, amani imshukie, na ndani yake akamuingiza Peponi, na ndani yake akamtoa na akamteremsha duniani, na Kiyama hakitosimama ila siku ya Ijumaa.