explain-icon

Ufafanuzi

Atakayegeuka kwa moyo wake au vitendo vyake au kwa vyote viwili katika kitu ambacho anataraji manufaa au kuzuia madhara, Mwenyezi Mungu humuwakilisha katika kitu hicho ambacho amekielekea, atakayemuelekea Mwenyezi Mungu humtosheleza na humfanyia wepesi kila zito, na mwenye kumuelekea asiyekuwa yeye Mwenyezi Mungu humfungamanisha katika kitu hicho na humfedhehesha.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Katazo la kuegemea kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  • Ulazima wa kuegemea kwa Mwenyezi Mungu katika mambo yote.
  • Kubainishwa madhara ya ushirikina na ubaya wa mwisho wake.
  • Malipo huendana na matendo.
  • Nikuwa malipo ya kitendo hurudi kwa mfanyaji yakiwa ya kheri au ya shari.
  • Kushindwa kwa mwenye kujiondoa kwa Mwenyezi Mungu na akatafuta manufaa kwa asiyekuwa yeye.