Alikuwa kwa mama wa Waumini Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Haulaa bin Tuwaiti radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, akatoka alipoingia tu Mtume rehema na amani ziwe juu yake. Aisha akasema kumwambia: Mwanamke huyu halali usiku, bali hukesha kwa kuswali. Akasema rehema na amani ziwe juu yake akipinga kijitiadhiki kwa mwanamke huyo juu ya nafsi yake: Halali usiku! Hebu shughulikeni na matendo mema kwa kiasi mnachoweza kudumu nacho, namuapa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu hachoki kuwapa waja wake wema wenye kumtii thawabu na malipo kwa utiifu wao na mema yao na amali zao njema mpaka wachoke na waache kufanya amali.