Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba Peponi kuna sehemu watu watakuwa wakikusanyika hapo, hapatokuwa na kuuza wala kununua, bali watakuwa wakichukua kutoka hapo wanachokitaka, watakuwa wakienda hapo kwa kiasi cha siku saba, utavuma upepo wa kaskazi, utatikisa katika nyuso zao na nguo zao, wataongezeka uzuri na urembo, watarudi kwa familia zao wakiwa wameongezeka uzuri na urembo, watasema kuwambia: Wallahi hakika mmezidi uzuri na urembo baada yetu, na wao watasema: Na nyinyi Wallah hakika mmezidi uzuri na urembo baada yetu.