explain-icon

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba siku moja kuna mtu mmoja alikuwa akitembea njiani akapita katika tawi mti wa miba likiwa barabarani likiwaudhi waislamu, akalivuta na akaliondosha njiani, basi Mwenyezi Mungu akamshukuru na akamsamehe.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Fadhila za kuondoa udhia njiani, na kwamba hilo ni sababu ya kuupata msamaha wa Mwenyezi Mungu.
  • Kutodharau matendo mema hata yakiwa ni madogo.
  • Uislamu ni dini ya usafi na kulinda mazingira na amani ya jamii nzima.