Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayeruzukiwa mabinti wawili au dada wawili, akawasimamia katika mahitaji na malezi na kuwaelekeza katika kheri na kuwatahadharisha na shari na mfano wa hayo mpaka wakakua na kubalehe; atakuja siku ya Kiyama akiwa yeye na Mtume rehema na amani ziwe juu yake mfano wa hivi viwili, akaunganisha vidole vyake viwili, kidole cha shahada na cha kati.