Anaeleza Nabii -Ziwe juu yake Amani- katika hadithil Qudsiy hii, kuwa yeyote atakayetahiniwa kwa kumkosa kipenzi chake miongoni mwa ndugu wa karibu au yeyote, atakaposubiri mwanadamu juu ya kuondokewa na yule aliyemteua na kumchagua na akaona kua huyu ndiye mwenye mahusiano mazuri na yeye, kama mtoto, au baba mdogo, au baba, au mama, au rafiki, anapomchukua Mwenyezi Mungu Mtukufu kisha mwanadamu akataraji malipo basi hana malipo mengine zaidi ya pepo.