explain-icon

Ufafanuzi

Amehimiza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- juu ya kutenda wema, na mtu asiudharau hata kama utakuwa kidogo, na miongoni mwake ni ukunjufu wa uso kwa kutabasamu wakati wa kukutana, ni lazima kwa muislamu alipupie hilo; kwa sababu hujenga kuwa na ukaribu na ndugu yako muislamu na huingiza furaha kwake.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Fadhila za kupendana kati ya waumini, na kutabasamu na bashasha wakati wa kukutana.
  • Ukamilifu wa sheria hii na kugusa kwake kila sekta, nakuwa imekuja na mambo yote ambayo yana masilahi kwa waislamu na kuunganisha umoja wao.
  • Himizo la kutenda wema hata kama ni kidogo.
  • Inapendeza kuingiza furaha kwa waislamu; kwani ndani yake kuna kuleta ukaribu baina yao.