explain-icon

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- katika baadhi ya nyakati zake anapotawadha anaosha kila kiungo katika viungo vya udhu mara mbili, anaosha uso ikiwemo kusukutua na kupandisha maji puani na mikono miwili na miguu miwili mara mbili.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Kilicho wajibu katika kuosha viungo ni mara moja moja na kinachozidi inapendeza.
  • Sheria ya kutia udhu mara mbili mbili katika baadhi ya nyakati.
  • Sheria katika kufuta kichwa ni mara moja.