Amebainisha Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- kuwa kuoga siku ya Ijumaa kumetiliwa mkazo ni sawa na wajibu upande wa kila aliyebalehe katika waislamu waliowajibikiwa na Ijumaa, Na asafishe meno yake kwa mswaki na mfano wake, na ajitie manukato kwa harufu yoyote nzuri ya uturi.